Thursday, November 24, 2011

WANAFUNZI WAKODI MABASI KWENDA SHOO YA SUGU.....

SHOO ya uzinduzi wa mix-tape ya Anti Virus inazidi kubamba, upo uwezekano ikajaza nyomi ambalo halijawahi kutokea kutokana na ahadi ya wanafunzi wa vyuo vikuu kwamba watakodi mabasi kwenda kwenye viwanja vya Chuo cha Ustawi wa Jamii, Kijitonyama, Dar.

Anti Virus itasababishwa na Vinega Novemba 26, 2011, kuanzia saa 12 jioni mpaka 6:00 usiku na katika kuhakikisha wanashuhudia makamuzi ya maana, wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Tumaini, wameahidi kukodi m
abasi matatu ya kuwasafirisha kwenda kwenye shoo hiyo.



Wanafunzi wa Tumaini Dar, wamemuandikia SMS, kinega mkuu ambaye ni Mbunge wa Mbeya Mjini (Chadema), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, wakimueleza kuwa madenti wa vyuo vikuu wapo naye katika harakati za kuwakomboa wasanii wa muziki wa kizazi kipya.
“Wanakuita Sugu… Sugu… Sugu…Sugu! Kaka sisi wanafunzi wa Tumaini University ya DSM, tumeamua kukodi mabasi matatu ya UDA ili kuja katika shoo yako na Vinega hapo Viwanja vya Ustawi wa Jamii,” ilisomeka SMS hiyo.

Mratibu wa shoo hiyo, Fred Mariki Mkoloni alisema kuwa jukwaa na muziki (sound) ni vya kiwango cha juu na kwamba kinachosubiriwa siku hiyo ni wasanii Anselm Ngaiza ‘Soggy Dog,’  Suma G, Mapacha, Dani Msimamo na wengine kibao wakiongozwa na Sugu kuwasha moto wa gesi. 

No comments:

Post a Comment