Thursday, May 9, 2013

WANAFUNZI WA UHASIBU ARUSHA(IAA) WATAKIWA KU APPLY UPYA ILI KUENDELEA NA MASOMO


Kutokana na Chuo kufungwa, Baraza la Uongozi wa Chuo katika kikao chake cha dharura cha tarehe 03 Mei 2013 kimeagiza wanafunzi wote kuanzia ngazi ya Cheti mpaka Stashahada ya Uzamili kuzingatia yafuatayo:
1. Kila Mwanafunzi anatakiwa kutuma maombi mapya ya kujiunga na Chuo.
2. Barua ya maombi hayo ipitishwe kwa Mkuu wa Wilaya anapoishi mwanafunzi. Kwa mwanafunzi wa Stashahada ya Uzamili ya Uhasibu barua yake ya maombi ipitie kwa Mhasibu Mkuu wa Serikali.
3. Katika maombi hayo mwanafunzi anaagizwa kueleza namna alivyoshiriki katika vurugu za tarehe 24 Aprili 2013.
4. Mwanafunzi awe amekamilisha malipo ya ada iliyobaki wakati anatuma maombi yake.
5. Mwisho wa maombi ni tarehe 16 Mei 2013.
Maombi yapelekwe kwa anwani ifuatayo:
Mkuu wa Chuo,
Chuo cha Uhasibu Arusha
S. L. P. 2798
Arusha.
08 Mei 2013