Wednesday, February 20, 2013

PICHA YA ZOMBI ILIYOCHORWA NA MWANAFUNZI WA FORM IV 2012


Katibu mtendaji wa Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA)  Dr Joyce Ndalichako akionyesha karatasi ya majibu ya mmoja ya watahiniwa wa kidato cha nne mwaka 2012.
Joyce Ndalichako adai Clouds FM imechangia yaliyotokea Kidato cha Nne!
- Adai walimpa 'Promo' kijana aliendika matusi na "Bongo Flavor" katika mtihani wake wa Kidato cha Nne Mwaka jana kwa kumfanyia interview katika moja ya vipindi vyake.
- Adai kuwa hatua hiyo ya Clouds FM imechangia uandikaji wa matusi kwa watahaniwa wa mwaka huu...
Endelea kusoma hapa    http://j.mp/ZfpPur

CHIBWA FT JURU - NISHAI


               

MAKALLAWAUKOO FT DOMOKAYA - NIENDE WAPI

                        

Tuesday, February 19, 2013

TECHNOLOGY HOW TO USE VLC AS VIDEO CONVERTER


VLC is one of the popular software for play video files. How many of you know that we can convert video files with VLC player. We are using different video converters to convert video files. Hereafter you don't need to download or purchase a separate software for video converting. I'll show you an easiest way to convert videos with VLC Media player.

Lets see how to convert videos using VLC media player.

On VLC Player Click Media

Select Convert/Save

You can select a video file to convert by clicking Add button

Now click on Convert/Save

A window will appear, in that window click on Browse and select a path to save the converted video file.

You can choose output video format under the Settings area. 
On destination file specify the destination or your output file by click Browse. After specify the destination point,
 


Change file format that u want,
Finally click on start
That's all u done.
Hope this blog helps u
...  Vinii  Skill@z...

MATOKEO KIDATO CHA NNE 2012

Kumekua na matatizo ya kupata matokeo kwa muda unaotakiwa' na hii ni kutokana na kuwa Server/Website ya NECTA inakua busy saana! Kuna link ya kukupeleka direct. Hii hapa chini

Monday, February 18, 2013

MATOKEO KIDATO CHA NNE 2012 HAYA HAPA


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa (MB) leo ametangaza rasmi matokeo ya Mitihani ya Kidato cha Nne, maarifa - QT.
TAARIFA YA MATOKEO YA MITIHANI YA MAARIFA (QT) NA KIDATO CHA NNE (CSEE)
ILIYOFANYIKA OKTOBA 2012  
1.0                 UTANGULIZI
Mitihani ya Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT) kwa mwaka 2012 ilifanyika nchini kote kuanzia tarehe 8-25 Oktoba 2012.  Napenda kuchukua nafasi hii kutangaza rasmi matokeo ya mitihani hiyo kama ifuatavyo :
2.0                 MTIHANI WA MAARIFA (QT)
2.1           Usajili na Mahudhurio
Katika Mtihani wa Maarifa 2012 watahiniwa waliosajiliwa ni 21,310 ambapo wasichana walikuwa ni 13,134 na wavulana ni 8,176
Jumla ya watahiniwa 17,137 sawa na asilimia 80.42 ya waliosajiliwa wamefanya Mtihani. 
2.2          Matokeo ya Mtihani wa Maarifa (QT)
Watahiniwa 5,984 kati ya 17,137 waliofanya mtihani wamefaulu Mtihani wa Maarifa (QT).
3.0                 MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2012
Jumla ya vituo 5,058 vilitumika katika kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 ambapo vituo 4,155 vilikuwa vya watahiniwa wa shule na vituo 903 vilikuwa ni vya watahiniwa wa kujitegemea.
3.1                 Usajili na Mahudhurio ya Watahiniwa
(a)           Watahiniwa Wote
Jumla ya watahiniwa 480,036 walisajiliwa kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wakiwemo wasichana 217,583 sawa na asilimia 45.33 na wavulana 262,453 sawa na asilimia 54.67.  Watahiniwa waliofanya mtihani wa Kidato cha Nne 2012  ni 456,137 sawa na asilimia 95.44. Watahiniwa 21,820 sawa na asilimia 4.55 ya watahiniwa wote waliosajiliwa hawakufanya mtihani.
(b)            Watahiniwa wa Shule
Watahiniwa wa shule waliosajiliwa ni 411,230 wakiwemo wasichana 182,978 sawa na asilimia 44.50 na wavulana 228,252 sawa na asilimia 55.50.  Watahiniwa wa shule waliofanya mtihani walikuwa 397,136 sawa na asilimia 96.57. Aidha, watahiniwa 14,090 sawa na asilimia 3.43 hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo utoro,  ugonjwa na vifo.
(c)             Watahiniwa wa Kujitegemea
Watahiniwa wa kujitegemea waliosajiliwa walikuwa ni 68,806 wakiwemo wasichana 34,605 sawa na asilimia 50.29 na wavulana 34,201 sawa na asilimia 49.71. Watahiniwa 61,001 wakiwemo wasichana 30,917 na wavulana 30,084  wamefanya mtihani wakati watahiniwa 7,730 sawa na asilimia 11.23  hawakufanya mtihani.
4.0                 MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE
(a)                 Watahiniwa wa Shule
Jumla ya watahiniwa wa shule 126,847 kati ya watahiniwa 397,136 waliofanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2012 wamefaulu. Wasichana waliofaulu ni 46,161 na wavulana ni 80,686.
(b)                Watahiniwa wa Kujitegemea
Idadi ya watahiniwa wa kujitegemea waliofaulu mtihani ni 16,112 kati ya watahiniwa 61,001 waliofanya mtihani.  Wasichana waliofaulu ni 6,751 na wavulana ni 9,361. 
5.0                 UBORA WA UFAULU KWA MADARAJA NA JINSI
Ubora wa ufaulu kwa kuangalia madaraja waliyopata watahiniwa wa shule unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 23,520 wamefaulu katika madaraja I – III ambapo kati yao wasichana ni 7,178 na wavulana ni 16,342.
Mchanganuo wa ufaulu kwa kila Daraja kwa jinsi kwa Watahiniwa wa Shule mwaka 2012 ni kama ifuatavyo:

Saturday, February 16, 2013

WORLD GARDEN JENGO KUBWA NA LENYE KLABU NDANI YA JIJINI LA ARUSHA

JENGO LA WORLD GARDEN
Jengo jipya la mikutano pamoja na ukumbi wa disco lililopo jijini Arusha maeneo ya Moshono barabara zamani ya Moshi - Arusha. Mkuu wa Mkoa wa Arusha Magesa Mulongo amewaasa Watanzania wazidi kuwekeza katika janja tofauti tofauti ili kuzidi kuuweka mkoa wetu katika hadhi, mandhari nzuri pamoja na kiuchumi. Jengo lina kumbi za kufanyia mikutano, sherehe na pia lina night club.

Thursday, February 14, 2013

NIKKI WA PILI FT JOH MAKINI & G NAKO - NJE YA BOX

                                

UVAAJI WA WATOTO KAMA MASTAA KWENYE RED CARPET TUZO ZA GRAMMY 2013

Rihanna

Beyonce

 Taylor Swift

Adele

Justin Timberlake

MAJINA YA WALIMU WAPYA WA SHULE ZA MSINGI 2012-2013

AJIRA MPYA YA WALIMU WA SHULE ZA MSINGI MWAKA 2012/2013
Walimu wote waliopewa ajira ya Ualimu serekalini ambao majina yao yametangazwa katika tovuti za Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na Ofisi ya Waziri Mkuu - Tamesemi, wanatakiwa kuripoti tarehe 01 Machi 2013 kwenye ofisi za Wakurugenzi wa Halmashauri walikopangiwa kwa ajili ya kupangiwa Vituo vya kazi. Hakuna mabadiliko ya vituo vya kazi yatakayofanywa. Mwalimu anatakiwa kwenda na vyeti vyake halisi vya Taaluma na cheti cha Kuzaliwa pamoja na nakala zake. Mwalimu ambaye hataripoti ifikapo tarehe 9 Machi 2013 atapoteza nafasi hiyo.

NB: WALIMU WALIOKWISHA AJIRIWA WARUDI KWA WAAJIRI WAO.

Fungua Link hiyo hapo chini