Thursday, December 15, 2011

MITIHANI YA DARASA LA SABA YACHAKACHULIWA

WANAFUNZI 9000 WAFUTIWA MATOKEO, HATA WALE
WATAKAOINGIA KIDATO CHA KWANZA KUPIMWA UWEZO TENA 

Gedius Rwiza na Raymond Kaminyoge
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi imetangaza matokeo ya mitihani ya darasa la saba ikieleza kuwa wanafunzi 9000 wamefutiwa matokeo kutokana na udanganyifu na hata wale ambao watapangiwa shule za sekondari wapimwa uwezo wao kabla ya kuanza masomo.  Akitangaza matokeo hayo jijini Dar es Salaam jana, Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Philipo Mulugo pamoja na mambo mengine, alisema kutokana na tatizo hilo, wanafunzi waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwakani, watapaswa kuchujwa upya.

WANAFUNZI 43 WATIMULIWA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM


CHUO Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kimewafukuza wanafunzi 43 na kuendelea kufuatilia nyendo za wengine tisa, baada ya kubainika kuwa walihusika katika matukio mbalimbali ya vurugu na uhalifu chuoni hapo. Kati ya wanafunzi hao, wanane walikuwa wamesimashiwa masomo kwa muda wa miezi tisa na 35 walisimamishwa ili kusubiri kumalizika kwa kesi zao zilizopo mahakamani.

DAH SNOOP DOG APIGA MSUBA JUKWAANI


MWISHO & MERYL WAFUNGA PINGU ZA MAISHA NCHINI NAMIBIA