Friday, November 4, 2011

WARAKA WA MH. GODBLESS LEMA KWA WATANZANIA JUU YA KWENDA KWAKE JELA...


WAARUSHA NA WATANZANIA WAPENDA
MABADILIKO KOKOTE KULE WALIPO ULIMWENGUNI
JELA NI MAHALI PA KUISHI KAMA SABABU YA KWENDA HUKO NI VITA DHIDI YA UONEVU, UKANDAMIZAJI WA HAKI NA UTU WA BINADAMU.
Wapendwa wapiga kura wangu na Watanzania wenzangu.
Sina wakati mgumu kuchukua maamuzi haya yanayotokea leo. Upendo huu nilio nao kwa watu wa Arusha na nchi yangu ni sababu ya msingi ya maamuzi haya. Nimetishwa mara nyingi, rafiki zangu wametishwa, jamii ya watu duni imeendelea kuishi kwa mashaka na matisho kwa muda mrefu.