Wednesday, December 28, 2011

MAFURIKO YAHAMIA MJI WA MOROGORO

Hali ilikuwa mbaya kwa waliolazimika kupata mahitaji yao sokoni hapo.
BAADA ya jiji la Dar es Salaam kukumbwa na mafuriko yaliyosababisha vifo vya makumi ya watu na kuharibu nyumba nyingi za wakazi wa jiji hilo, mchana wa leo hali hiyo imehamia mkoani Morogoro ambapo baadhi ya nyumba za watu, likiwemo soko kuu la Manispaa ya Morogoro yamekumbwa na mafuriko makubwa kufuatia mvua kubwa zilizonyesha kwa muda wa dakika 45 mfululizo.